Tuesday, March 21, 2017

RATIBA KAMILI YA MECHI ZA MCHUJO WA KUWANIA  KUINGIA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO

RATIBA KAMILI YA MECHI ZA MCHUJO WA KUWANIA 
KUINGIA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO
Yanga SC (Tanzania) vs MC Alger (Algeria)
TP Mazembe (DRC) vs JS Kabylie (Algeria)
AC Leopards (Kongo) vs Mbabane Swallows (Swaziland)
FUS Rabat (Morocco) vs MAS Fez (Morocco)
Rangers (Nigeria) vs Zesco (Zambia)
Mounana (Gabon) vs ASEC Mimosas (Ivory Coast)
RC Kadiogo (Burkina Faso) vs CS Sfaxien (Tunisia)
Bidvest (Afrika Kusini) vs Smouha (Misri)
CNaPS (Madagascar) vs Recreativo do Libolo (Angola)
KCCA (Uganda) vs El Masry (Misri)
Ports Authority (Gambia) vs Hilal Obeid (Sudan)
Port Louis (Mauritius) vs Club Africain (Tunisia)
Rivers United (Nigeria) vs Rayon Sports (Rwanda)
BYC (Liberia) vs Supersports (Afrika Kusini)
AS Tanda (Ivory Coast) vs Platinum Stars (Afrika Kusini)
Horoya (Guinea) vs Ittihad Tangier (Morocco)

(Mechi za kwanza zinatarajiwa kucheza wikiendi ya Aprili 7 hadi 9 na marudiano yanatarajiwa kuwa wikiendi ya Aprili 14 hadi 16, mwaka huu)


Sunday, March 19, 2017

JIFAHAMU HUENDA UNATATIZO LA PRESHA YA KUPANDA AMA YA KUSHUKA


PRESHA YA  KUPANDA.
Hii hutokea pale nguvu ya msukumo wa damu inayosukumwa na moyo kwenda kwenye mishipa ya damu(Arteri) kuwa kubwa kuliko njia ya mishipa hiyo hivyo kushindwa kuhimili nguvu au mgandamizo huo wa damu,unaweza kuwa na tatizo hili la mgandamizo mkubwa wa damu(Hypertension) kwa mda mrefu bila kuhisi dalili zozote na kupelekea uharibifu wa mishipa ya damu kuzid kuendelea hadi kusababisha Shinikizo la damu(Heart Attack).

presha ya kupanda ni 140mmHg juu yaani pale mgandamizo wa damu unapozid wakati 90mmHg ni pale moyo unapojilegeza na kujaza damu kama visemavyo vipimo ya tatizo hii..Kwamba
~Presha ya kawaida(Normal) ni 120/80mmHg
~Presha ya kupanda(Hypertension)
Stage 1) 140/90mmHg
Stage 2) 160/100mmHg
Stage 3) 180/110mmHg
Presha kubwa zaidi(Hypertensive Crisis)     240/120mmHg.

SABABU ZA PRESHA YA KUPANDA

A) STAILI YA MAISHA
i) Kutojishughulisha/Uvivu.
ii) Chumvi nyingi kwenye chakula cha kusindikwa na chenye mafuta.
iii) Pombe na uvutaji wa Sigara.
iv) Chakula kisicho na madini ya Pottasium ya kutosha.

B) UMRI
i) Umri unapozidi kuwa mkubwa kuanzia miaka 60 kunauwezekano wa kupata tatizo hili.

C) JINSIA
-Wanaume wapo hatarini kupata kwenye umri mdogo wakati Wanawake hupatwa zaidi wanapokuwa na umri mkubwa.

D)KURITHI.

E)UZITO MKUBWA.

F)MSONGO WA MAWAZO.

DALILI ZA PRESHA YA KUPANDA

i) Kizunguzungu.
ii) Kichwa kuuma.
iii) Kutoona vizuri.
iv) Kichefuchefu.
v) Kubanwa na Pumzi.

MADHARA YA MGANDAMIZO MKUBWA WA DAMU.

i) Uvimbe mkubwa kwenye kuta za arteri(Aneurysm).
ii) kupanuka au kudhoofika kwa moyo hadi kufikia kishindwa kusukuma damu ya kutosha(Heart Failure).
iii) Kusinyaa kwa mishipa ya damu kwenye figo na moyo kusababisha vishindwe kufanya kazi,ubongo na miguu pia.
iv) kupasuka kwa mishipa ya damu na kusababisha macho kutoona Vizuri au Upofu kabisa.

*PRESHA YA KUSHUKA(HYPOTENSION)*
Hii hutokea pale mgandamizo wa damu usukumwao na moyo kupitia kwenye njia au kuta za mishipa ya damu(Arteri) kuwa mdogo kuliko upana wa mishipa yenyewe hivyo kupelekea damu chache kufika kwenye ubongo,figo na sehem nyingine za viungo mwilini.
Mfano wa Viwango Vyake ni:
     * 90/60mmHg.
     * 115/60mmHg.
     * 115/50mmHg.

DALILI ZA PRESHA YA KUSHUKA.

i)Kizunguzungu na kuanguka.
-Hii hutokana na damu kufika kidogo kwenye ubongo hasa pale unapokuwa na tatizo la kiafya.

ii) Mapigo ya moyo kuongezeka.
-Hii ni hasa pale unapokuwa umeketi na kuinuka ghafla kiwango cha damu yako kinakuwa kimebaki sehem ya chini Miguuni na endapo hakutakuwa na hatua yoyote kuchukuliwa na mwili wako husababisha presha yako kushuka na ikiwezekana kudondoka ghafla na hata kuzimia pia.

iii) kushindwa kuzingatia vzuri jambo
-kutokuwa makini eitha na taarifa muhimu upewayo au jambo muhimu la kulifanyia kazi.

iv) Kujihisi kuchoka choka sana na kutapika.

v)Kuvuta pumzi kwa taabu.

AINA ZA PRESHA YA KUSHUKA.

I)ORTHOSTATIC HYPOTENSION.
-Hutokana na kubadili mazingira uliyonayo kwa ghafla mfano.kusimama ghafla kutoka ulipokaa au ulipo lala na huwa haichukui mda mrefu ni sekunde kadhaa mpaka dakika moja.

II)NEURALLY MEDIATED HYPOTENSION(NMH).
*Huwapata zaidi vijana na watoto kutokana na÷
             -Utumiaji wa pombe.
             -Utumiaji mkubwa wa dawa                         za presha ya juu(ya kupanda).
             -Utumiaji wa dawa za nusu kaputi wakati wa kufanyiwa Oparesheni.

III) SEVERE HYPOTENSION.
*Hutokana hasa hasa na kupoteza fahamu.

HALI INAYOSABABISHA PRESHA HII

i) Kuwa na mimba.
ii) Matatizo ya hormoni mwilini(Hormone imbalance).
iii) Maradhi ya Kisukari.
iv) Utumiaji mkubwa wa dawa za hospitali zikiwamo za presha ya kupanda.
v) Maradhi ya Moyo.

*KWA USHAURI ZAIDI JUU YA UTATUZI WA TATIZO HILI LA PRESHA TUWASILIANE KWA
0715 280 233.
0769 280 233.
0625 738 210.

Whatsapp number 0715 280 233*


Sunday, March 12, 2017

TAHADHARI MAMA UNATUMIA TAA ZA ENERGY SAVER..

Tunapenda kupunguza matumizi ya nishati, hizi bulb ambazo ni rafiki wa mazingira na zinazookoa nishati(energy serving bulb) zimekuwa zikitumika zaidi kwa sasa.

Ila ni vyema ujue kwamba hizi bulb za kisasa ni kweli zina sumu. Shirika la kulinda Mazingira limetoa maelekezo ya dharura unayohitaji kuyafuata endapo bulb yako itavunjika.

Hii ni kutokana na gesi yenye sumu inayotoka endapo bulb itavunjika.

Taasisi ya Fraunhofer Wilhelm Klauditz ya Ujerumani inadai kuwa kama taa hii itavunjika ndani ya nyumba itatoa mara 20 zaidi ya Mercury katika hewa

Bulb hizi za kupunguza matumizi ya Nishati zinaweza kukuletea matatizo haya;

KizunguzunguKifafaMaumivu ya kichwaUchovuKutostahimiliWasiwasi

1.Bulbu hizi zinazookoa nishati zina wingi wa zebaki(mercury)

Mercury ni hatari hasa kwa 

watoto na wanawake wajawazito. Uharibu mfumo wa neva, ubongo, figo na ini.Pia uharibu uzazi, kinga ya mwili, mfumo wa mishipa ya moyo,pia inaweza kukusababishia mitikisiko,kukosa usingizi, kuumwa kichwa, wasiwasi na kupoteza kumbukumbu 

2.Bulb hizi zinaweza kukusababishia Kansa

Utafiti uliofanywa Maabara uligundua kwamba hizi balbu pia zina sumu zinazoweza kukusababishia kansaPhenol, tindikali hii yenye chembechembe nyeupe zenye sumu inapatikana katika makaa ya mawe na inatumika kwa matumizi ya viwandaTaa hizi zina wingi wa mionzi ya UVMionzi hii ya UV si mizuri kwa afya ya ngozi na inaweza kukusababishia kansa ya ngozi.

Baada ya kusoma haya maelezo unaweza kuchagua kuendelea kutumia balbu hizi kwa maana gharama zake ni nafuu, kama utafanya hivyo basi yakupasa kusoma maelekezo na kujua jinsi ya kukabiliana na mercury(zebaki) na kemikali zinazoweza kukusababishia kansa.

Fanya hivi kabla ya kutoa bulb iliyopasuka;


Watu na wanyama waondoke katika chumbaFungua madirisha na milango kwa mda wa dakika 5-10


Saturday, March 11, 2017

VIPODOZI UTUMIAVYO NI SALAMA KWA AFYA YAKO?

ZIFUATAZO NI FIKRA POTOFU KUHUSU NGOZI YAKO NA VIPODOZI
1. Kipodozi ambacho kinachubua ngozi ndicho huitwa kipodozi chennye KEMIKALI. Hii fikra potofu ina angamiza afya za watu ungana name ujue kipodozi kipi ni kemikali na kipi sio cha kemikali.
2. Kupatwa kwa chunusi uso mzima ambazo zinashamiri kila siku kuhusisha vipodozi unavyotumia na hatimaye kubadili vipodozi kila siku. Leo hii utajifunza namna gani sumu katika mfumo wa chakula husababisha chunusi sugu na namna gani ya kuondoa tatizo na kukuepusha hatari ya kubadili vipodozi kila siku.
3. Kubadili vipodozi kila mara kwa dhumuni la kuondoa chunusi sio suluhisho kwa ngozi yako.

KIPODOZI CHA KEMIKALI NI KIPI?

Hiki ni kipodozi ambacho kina kiambata ambacho kinaweza kuathiri afya ya binadamu na kusababisha magonjwa na hatimaye ulemavu wa kiafya. Sio kweli kwamba vipodozi vyenye kemikali ni vile tu vyenye KUCHUBUA NGOZI YAKO bali vipodozi vingi tu vimekuwa vikipewa jina la kibishara kuwa ni vya ASILI na sisi watumiaji hutumia bila kuangalia kuwa vina viambata gani ambavyo haviwezi kudhuru miili yetu.

VIPODOZI VYA ASILI NI VIPI?

Hivi ni vipodozi ambavyo vimetokana na vitu asili ambavyo havina mathara kwa kumtumiaji na haviwezi kubadili utendaji kazi wa mwili pia afya ya mgonjwa. Vinaweza kutokana na mimea,matunda na wanyama pia mazao yatokanayo na wanyama kama asali, mafuta nk

VISABABISHI VYA CHUNUSU SUGU 
Ni dhahiri kuwa watu wengi tunajua kuwa chunusi husababishwa na utengenezwaji wa mafuta mengi ya sebum ambayo hutengenezwa na tezi iliyopio chini ya ngozi. Mafuta haya yakizidi kiwango huweza kuziba vitundu vidogo vya ngozi na hatimaye ngozi kutopumua vizuri kwani haitaweza kupitisha jasho ipasavyo na hatimaye kutengeneza mkusanyiko wa uchafu kwenye njia ya jasho. Mkusanyiko huu unaweza kuvamiwa na bacteria na hatimaye usaha kutungwa. Lakini hii sio kisababishi kikubwa cha chunusi sugu kwetu sisi binadamu ingawaje pia ni moja wapo ya kisababishi. Zingatia yafuatayo kama visababishi vikubwa vya chunusi sugu
1. Kuzidi kwa vichocheo vya androgen mwilini. Hivi ni vichocheo vinavyo shughurika na uzazi endapo vinapozidi husababisha utengenezwaji wa mafuta ya sebum kwa wingi. Vichocheo hivi huongezeka hasa wakati wa kubarehe ndio maana wengi chunusi hushamiri sana kipindi hiki. Lakini vichocheo hivi huweza kuvurugwa na utumiaji wa vyakula vyenye sukari sana kama soda, na vyakula vingine vya viwandani kama mikate, sambusa, danati na vingine vingi. Hivyo watu wengi hupatwa na matatizo ya chunusu sugu hasa ndogo ndogo hii ni kutokana na mvurugiko wa vichocheo hivi kutokana na maisha tunayo ishi nayo. Kitendo cha kutibu chunusu kwa kutumia sabuni za kupunguza mafuta ni dhahiri kuwa unaweza kupata nafuu lakini tatizo halitakwisha. Hivyo kuhakikisha kuwa unatibu tatizo la mvurugiko wa vichocheo hivi ndipo suluhisho la chunusu sugu litakuwa limeisha.
2. Kuchafuka kwa mfumo wa chakula kutokana na sumu kama mercury, arsenic na sumu zingine nyingi ambazo huathiri mfumo wa chakula mzima. Pia utumiaji wa vyakula vya ngano vyenye kwani vina protini iitwayo GLUTEN kwani ndio kisababishi kikubwa cha cha mfumo wa chakula kutofanya kazi ipasavyo na hatimaye kuharibu mifumo mingi ya utendaji kazi wa mwili. Hivyo watu wengi ambao hupata chunusi vidogo vidogo kama allergy kisababishi kikubwa ni utumiaji wa vyakula vya ngano vyenye GLUTEN.
3. Utumiaji vyakula vya sukari nyingi kwani ndio kisababishi kikubwa cha kuongezeka kwa sukari mwilini na kusabaisha insulin kuongezeka kwenye mzunguko wa damu. Kuongezeka kwa insulin huharibu vichocheo vingine na hatimaye kusababisha madhara makubwa ya mwili katika ndozi yako. Hapa ndipo utakuta watu wanene kupita kiasi haishiwi na vipele vidogo vidogo usoni hii ni kutokana na kwamba ameanza kupata dalili za mwanza za kisukari aina ya pili kwani ni ishara kuwa insulin haifanyi kazi ipasavyo.

4. Maambukizi kwenye ngozi. Kuna watu ambao imekuwa ni kawaida yao pindi tu wanapopatwa na chunusi huenda madukani kununua cream zenye antibiotics kama TETRACYCLINE CREAM, getriderm Na wengine hukimbilia kununua cream kama SONADEMA na nyinginezo. Unachotakiwa kujua ni kwamba sio kwamba hizi tube ni mbaya la hasha!!! Tube hizi zinashauriwa kutumika pale tu unapokuwa na chunusi zenye kutunga usaha. Hivyo tunakushauri utumie antibiotics cream hizi. Hivyo tufuate mashati ya matumizi ya dawa hizi zenye kemikali tuachane na matumizi mabovu na fikra potofu kila chunusi lazima uende phamarcy.

5. Mchafuko wa damu. Kama wewe huwezi kuondolea mwili sumu zinazo ingia mwilini kupitia ngozi, hewa, chakula mwili utaanza kuzito hizo sumu kupitia ngozi. Hivyo kuchafuka kwa ngozi yako ni dalili moja wapo kuwa umelemewa na sumu nyingi mwilini mwako unatakiwa kuzitoa tu hizo sumu kwa kutumia viondoa sumu yani anti oxidant. Hivyo kitendo cha kubadili vipodozi kila siku kwa dhumuni kuwa vimekukataa ni upotevu wa mali na kudhizidi kuingiza sumu zingine mwilini kupitia ngozi hiyo hiyo.

Basi leo ningependa nizungumzie sumu au kemikali ambazo zipo kwenye vipodozi vyetu vya kila siku na madhara yake. Kwani nimeamua kufanya hili baada ya kugundua kuwa watu hawajui nini hasa ya neon kipodozi chenye kemikali. Wengi wetu wamekuwa wakifikili kuwa kipodozi chenye kemikali ni kile ambacho kinachubua ngozi pekee lakini ukweli utajibiwa na maelezo yafuatayo kwa kina yanayo elezea jinsi vipodozi vingine ambavyo havichubui lakini vimebeba kemikali zinazo hatarisha afya zetu

ZIFUATAZO NI AINA ZA KEMIKALI ZINAZO HATARISHA AFYA ZETU KWENYE VIPODOZI

Vipodozi vyenye kemikali hupimwa ukali wa kemikali iliyomo humo kwa kutumia kipimo kiitwacho ENVIRONMENTAL WORKING GROUP au EWG. Hiki ni kipimo kinacho onesha uwezo wa kemikali kudhuru afya ya binadamu. Hiki kipimo kina madaraja makuu matatu yanayo onesha ukali wa kemikali husika kwenye kipodozi au vyakula kama ifuatavyo

1. EWG 0-2- ina madhara kidogo kwa binadamu
2. EWG 3-6- ina madhara ya kati kwa binadamu
3. EWG 7-10 – Inamadhara makubwa kwa binadamu.

Baada ya kuona madaraja ya kubaini viwango vya madhara vya kemikali mbali mbali kwenye vipodozi kulingana na ENVIRONMENTAL WORKING GROUP. Basi hebu naomba tuongelee kemikali mbali mbali zilizopo kwenye vipodozi vyetu vya kila siku na viwango vyake na madhara yake.

1. 1,4 DIOXINE
Hii ni kemikali amabayo hutumika kupunguza sumu ya kemikali kali ambazo zinatumika kutengeneza vipodozi au bidhaa yoyote kwa matumizi ya ngozi.
Ina kiwango cha EWG cha 8 tafsiri yake ni sumu kali zaidi 

MADHARA YAKE

a) Inasababisha kansa yani ni CARCINOGENIC kwani ina uwezo mkubwa wa kubadilisha seli za binadamu na kuwa kansa.
b) Ina ua figo yako yani ni kidney toxicant
c) Ina angamiza mfumo wa fahamu wa binadamu hasa ubongo na kusababisha magonjwa ya kusahau ovyo
d) Ina sababisha magonjwa ya mfumo wa upumuaji kama asthma ya ukubwani kutokana na madhara yake katika mapafu

INAPATIKANA WAPI

Aina hii ya kemikali ipo kwa wingi sana katika SHAMPOO na BODY LOTION tunazo tumia kila siku na kusema kuwa ni alama kwani hazichubui.
SOMA HAYA KUJUA KUWA KIPODOZI HIKI KINA 1,4 DIOXINE
a) Vipodozi vyote vyenye viambata hivi, eth, myreth,oleth,laureth na ceteareth ukiona hivi ujue kuwa hii kemikali ilitumika kuziandaa hizi kwa kuzipunguzia makali ya sumu.
b) Vipodozi vyenye PEG
c) Vipodozi vyenye, polyethylene glycol
d) Vipodozi vyenye, polyoxyethylene na Oxynol
Vipodozi vyote vyenye ingredient kama hizo ujue kuwa zina hii kemikali ambayo hadi sasa inaangamiza dunia kwa kutojua elimu hizi.

2. PARABENS

Hii ni aina ya kemikali ambayo ukichunguza kila vipodozi vina hiki kiini. Ili uweze kuhakikisha ni kuwa chunguza kwa makini vipodozi vyako itaikuta ipo katika mifumo aina kuu nne kama ifuatavyo
a) Methyl parabens: EWG 4
b) Ethyl parabens: EWG 4
c) Propyl parabens :EWG 7
d) Isobutyle parabens: EWG 7

MADHARA YAKE

Kemikali ya PARABEN ina uwezo mkubwa wa kuharibu mfumo wa vichocheo vya mwili yani HORMON. Kwani ndiyo kisababishi kikubwa cha kuvurugika na kuongezeka kwa vichocheo vya kike vya estrogen na kupelekea kuwa na maumivu wakati wa hedhi na matatizo mengine yote wakati wa hedhi. Pia husababisha kutokea kwa vimbe kama uvimbe wa titi na uvimbe kwenye kizazi

INAPATIKANA WAPI?
1. DEODORANT SPRAY
2. MAKE UPS
3. SHAMPOO
4. LOTIONS 
5. VIONJO KWENYE VYAKULA VYA VIWANDANI
6. DAWA ZA KEMIKALI
NOTE: Soma kwa makini mafuta yako ujue kuwa kemikali hii haipo kwani ndio suluhisho pekee la kuishi bila magonjwa sugu tafadhari kuhudhuria hospitali sio tiba bali kuepuka vitu kama hivi ndio tiba pekee

3. PHTHALATES
Kuna aina kuu nne kama ifuatavyo
a) Diethylhexyl phthalates EWG10
b) Dibutyl phthalates EWG 10
c) Dimethyl phthalates EWG 4
d) DiEHTYL PHTHALATES EWG 3
MADHARA
Inamaliza nguvu zakiume kwa kupunguza kiwango cha testosterone hormone pia ina punguza kiwango cha mbegu zakiume.
INAPATIKANA KATIKA MAJI YA KEMIKLI YA KUSAFISHIA NGUO,CHOO AU GARI, VIFAA VYA PLASTIC VINGI HUTENGENEZWA KWA HII CHEMIKALI
4. TOLUENE EWG 10
Hii aina ya kemikali hupatikana kwenye rangi mbalimbali za kupakalia majumba na vyombo mbali mbali
MADHARA
Matumizi ya mara kwa mara au kutumia kwa muda mrefu yanaweza kusababisha figo yako kuharibika,ini kuugua na kinga ya mwili kushuka

5. TICLOSAN
Hii kemikali hupatikana kwa wingi sana katika sabuni tunazo ogea kila siku. Hasa sabuni zilizo andikwa ANT BACTERIAL SOAP. Angalia kwa makini. 
MADHARA
Huvuruga hormone za kike,figo kufa na magonjwa ya moyo.
ANGALIA KOPO LAKO KWA MAKINI KWANI NINA IMANI KUEPUKANA NA HIVI VITU KUTAPUNGUZA GHARAMA ZAKUONANA NA DAKTARI KILA SIKU,KUPOTEZA MUDA WAKAZI UKIHANGAIKA KUTIBU UGONJWA NA KUPOTEZA NGUVU KAZI YA FAMILIA YAKO.

SOMA KWA MAKINI INGREDIENT ZA MAKOPO YAKO UNAPOSOMA ZINGATIA UJUMBE HUU

“Ushauri wangu ni kwamba tuache kupeperusha bendera ya umagharibi (kuiga tamaduni za kigeni), tudumishe mila zetu ikiwemo kula vyakula vya asili, matatizo haya yatapungua kwa kiasi kikubwa,” DR MERCOLA

Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza alinukuliwa wakati mmoja akisema mamlaka hiyo imepiga marufuku vipodozi vyote vyenye viambata sumu, lakini watu wanaendelea kuvitumia.

“Madhara yake ni makubwa, mwanamke mjamzito ni rahisi kuzaa mtoto taahira, au mimba ikatoka,” alisema huku Daktari wa Magonjwa ya Ngozi wa Kituo cha Afya Centre, Isaack Maro akisema wanawake wanaotumia vipodozi vyenye viambata sumu huathirika kwa kiasi kikubwa bila kujijua.
Alisema madini ya zebaki yanayotumika katika vipodozi vingi hayatoki kwa urahisi mwilini kwani hujazana mwilini kwa muda mrefu na kusababisha maradhi.
VIPODOZI HATARI ZAIDI KWA MTUMIAJI : MISS AFRICA, CITROLIGHT, COCODERM, CAROLIGHT, MAXLIGHT, EXTRA CLAIR, TOP LEMON PLUS, BETA SOL LOTION, LEMONVATE CREAM, JARIBU KWANZA, DIPLOSON, SUPER CLAIR, CLAIR MEN, FAIR AND HANDSOME, BIOCLARE, CAROTONE, MEDICATED FADE CREME, PRINCESS CLAIR, EPIDERM, BETASOL, IVAN HABART na SICAIRE.

……..IF YOU CAN”T PRONOUNCE THEM,THEY ARE PROBABLY NOT GOOD FOR YOU……..

REFERENCES
1. Environmental working group website
2. Who recommendations on skinny healthy products
3.The china study by Prof collin campbell


Hatarii...Kafulila Aingia Katika Vita ya Makonda,Amtaka Aonyeshe Vyeti Vyake ...!!!!

Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ameibuka na kuongea mambo matano kuhusiana na sakata la vyeti feki linalomuandamana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.Kafulila amesema yafuatayo;

"Kwanza ni ushauri wangu kwamba Makonda amsaidie Rais ama kwa kuonesha vyeti vyake vyote kuondoa utata au ajizulu ili serikali iendelee na mambo mengine. 

"Obama alipotuhumiwa kuhusu uraia wake USA alifanya kazi ndogo tu ya kuweka vyeti vyake vyote hadharani na akawa amefunga utata wa uraia wake. hivyo ni vema Makonda afanye hivyo kama anavyo au akae pembeni kwani nchi ni muhimu kuliko mahusiano yake na Rais.

"Rais anapaswa kujua kuwa hoja ya jinai ya kughushi vyeti inayopigiwa kelele inahusu pia umakini wa mamlaka yake kama mteuzi wa Makonda kwamba kuna shida ya vetting. hivyo kuondoa hilo ni kuchukua hatua stahiki. hakuna namna Rais atamlinda Makonda na akabaki na sifa ya kuwa Rais anaesimamia haki na Usawa. Itafanya aonekane kama waliomizwa na ukali wake katika kusimamia sheria ni kwasababu hawakuwa na ukaribu nae na zaidi itafanya aonekane Rais wa kawaida sana kwa kulinda uovu kwa sababu za binafsi.Hivyo ukimya wa Rais unafanya dhamira yake ya uzalendo ihojike kwani sio kawaida yake.

"Mamlaka kama Sekretariet ya Maadili ya Uongozi ilipaswa kuwa imeshachukua hatua kuondoa wingu hili kwani kinachojadiliwa hapa mbali zaidi ya jinai pia kinahusu uadilifu wa Kiongozi(intergrity). ukimya wa taasisi hii ni mfano mbaya wa namna taasisi zinavopigwa ganzi pindi haki inapotakiwa kutendeka lakini inagusa maslahi ya Rais. huu ni uzoefu niliopata kuona hata kwenye sakata la Escrow.likitokea jambo ambalo Rais ana maslahi taasisi zetu zimekuwa nzito na kigugumizi kuchukua hatua ipasavyo.

"Chuo cha Uvuvi walichomsajili kwa cheti cha form4 ambacho anatuhumiwa kuwa sio chake pamoja na Chuo Kikuu ni taasisi ambazo mjadala huu unahusu heshima ya taasisi hizo. hivyo ilipaswa zijitokeze kuthibitisha au kukanusha. ukimya wao unaashiria hofu yao kwasababu kaguswa mtoto wa mfalme! Huu ni mfano mbaya kabisa kwa taasisi za taaluma kwamba zinaweza kuwa za hovyo kiasi hiki.

"Kibaya zaidi ni ukimya wa NECTA ambao ni mamlaka ya kutoa vyeti. sasa cheti kinachosumbua hapa ni cha form4 ambacho ni mali yao. lakn kwa woga wamekaa kimya kuficha ukweli na kuacha mjadala wa cheti uwe kati ya Askofu na RC na watanzania wakati wao ambao ni mamlaka sahihi kuondoa utata wamekaa kimya kwa hofu ya kugusa mtoto wa mfalme.. Hili ni fundisho la kwani nchi hii haiendelei kwasababu taasisi hizi haziko imara kutimiza majukumu yake kisheria bali zinafanya majukumu yake kwa kadiri ya mapenzi ya mteule wao."