
Saturday, August 15, 2015
Yafahamu Madhara ya Ulaji wa Chumvi kupita kiasi Mwilini

Yafahamu Magonjwa Sugu ya Njia ya Hewa, Chanzo chake na jinsi Kuishi nayo

HATARI: Vimelea vipya vya Kisonono Visivyotibika kama Virusi vya Ukimwi vyagundulika

Dalili za Ugonjwa wa Uvimbe wa Tezi za Uzazi kwa Wanawake na Tiba yake

Wanaotoa Mimba chini ya Miaka 18, hatarini kupata Ugonjwa wa Saratani ya Shingo ya Kizazi

Unataka kutumia Vidonge vya Uzazi wa Mpango Kuzuia Mimba? Jiandae na Madhara 10 haya
Vidonge vya Uzazi wa Mpango, ni moja ya njia inayopendekezwa na Wataalamu wa Mpango wa Uzazi katika kuzuia mimba. Hata hivyo, vidonge hivyo vinaweza kutimiza malengo hayo ya mpango huo ikiwa tu vitatumiwa vizuri na kwa usahihi, kwa sababu tafiti zilizopo, zinaonyesha kwamba asilimia nane (8%) ya wanawake hupata mimba zisitarajiwa kila mwaka, huku wakiwa katika mpango huo kutokana na baadhi yao kujisahau kumeza vidonge hivyo.
Kwa mujibu wa tafiti
, vidonge hivyo vya mpango wa uzazi vikitumiwa vizuri, kwa kuhakikisha muda wa matumizi yake unakuwa ule ule, ni mwanamke mmoja pekee kati ya 100 anayeweza kupata mimba isiyotarajiwa ndani ya mwaka wa kwanza wa matumizi ya dawa hizo.
Hadi sasa kuna aina kuu mbili tu za vidonge vya uzazi vinavyotumiwa na wanawake katika wa mpango huo, ingawa aina zote hizo zina vichocheo (hormons). Aina hizo kitaalamu zinaitwa Estrogen na Progesteron. Estrogen ni aina ya kichocheo kinachotengenezwa na uterasi/kizazi, kinachosaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi, kwa kuongoza ukuaji wa kuta za uterasi kwenye sehemu ya kwanza ya mzunguko wa hedhi.
Kwa upande wake, Progesteron, hiki ni kichocheo cha kopasi luteamu ya ovari, kinachosaidia kuanzisha mabadiliko katika endometriumu baada ya ovulesheni.
Ingawa katika aina hiyo mbili ya vidonge, kuna vingine vina kichocheo cha aina moja tu, kwa maana ya ama Estrogen au Progestron, huku vingine vikiwa na vichocheo vyote viwili hivyo, lakini vidonge vyote hivyo ni salama, na vinafanya kazi kwa kufanya ute mzito kwenye shingo ya mji wa mimba na kuzuia kupevuka kwa yai, hivyo kuzuia mimba kwa kiwango cha asilimia 99.
Vidonge vya uzazi wa mpango vinaweza pia kutumika kama tiba ya kuweka sawa mzunguko wa hedhi, kuzuia maumivu makali wakati wa hedhi, kutibu chunusi pamoja na kupunguza hatari ya magonjwa katika via vya uzazi, ambayo hayatokani au kusababishwa na magonjwa ya ngono.
Hata hivyo, pamoja na usalama wa vidonge hivyo katika kufanya kazi yake hiyo ya kuzuia mimba na tiba kwa magonjwa hayo, vidogo hivyo vinaweza kumsababishia athari za kiafya mwanamke kama havitumiki katika mpangilio sahihi. Athari kuu 10 zinazoweza kusababishwa na vidonge hivyo ni pamoja na kutokwa na damu ukeni baada ya hedhi ya kawaida.
Kwa mujibu wa wataalam wa mpango huo, athari hiyo huweza kuwapata asilimia 50 ya wanawake wote wanaotumia vidonge vya uzazi wa mpango. Hali hii huweza kuwatokea ndani ya miezi mitatu baada ya kuanza matumizi ya dawa hizi. Kwa ujumla, hali hiyo huweza kukoma kwa zaidi ya asilimia 90, pindi mwanamke anapoanza kutumia pakti ya tatu ya dawa hizo katika kipindi hicho cha kutokwa damu ukeni.
Mwanamke anapotokewa na hali hiyo kwa mfululizo wa siku tano au zaidi baada ya kumaliza siku zake za kawaida za hedhi, anashauriwa kuwasiliana na mhudumu wa afya wakati akiendelea kutumia dawa hizo.
Athari ya pili, ni kujisikia kichefuchefu. Mara nyingi hali hiihumtokea mwanamke mwanzoni tu baada ya kuanza kumeza vidonge vya uzazi wa mpango, ingawa hali hii inaweza kukoma baada ya siku chache. Inashauriwa pia kwa mwanamke anayepatwa na hali hii ya kichefuchefu kuwasiliana na mhudumu wa afya kama ataona hali hiyo inazidi. Matiti kujaa au kuwa na maumivu, ni athari nyingine inayoweza kusababisha na matumizi ya vidonge hivyo. Hali hii huweza kumpata baada ya kuanza kutumia vidonge hivyo, na huweza kukoma ndani ya wiki moja tu.
Hata hivyo, inashauriwa kwamba ikiwa matiti hayo yatatokwa na uvimbe au maumivu yasiyoisha, ni muhimu kutafuta tiba kwa wahudumu wa afya, ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi ya kinywaji chenye kafeini na chumvi na kuvaa brauzi isiyobana matiti.
Maumivu ya kichwa ni athari nyingine inayoweza kumtokea mwanamke, ingawa pia kuumwa kichwa kunaweza kuwa na dalili za magonjwa mengine. Hata hivyo, kama itatokea maumivu hayo ya kichwa yakaanza tu mara baada ya kumeza vidonge hivyo, hiyo itakuwa ni dalili ya athari mojawapo na ni vyema kutoa taarifa kwa mhudumu wa afya.
Vidonge vua uzazi wa mpango huweza pia kuongezeka uzito wa mtumiaji, ingawa tafiti nyingine zimeshindwa kuthibitisha uhusiano kati ya vidonge hivyo na mabadiliko ya uzito wa mtumiaji. Aidha, baadhi ya wanawake hupatwa na tatizo la maji kuganda kwenye matiti na maeneo ya nyonga baada ya kutumia vidonge hivyo.
Mabadiliko ya hisia huweza pia kumtokea mwanamke anayeanza kutumia vidonge vya uzazi wa mpango. Inashauri kwamba pindi mwanamke anapoona dalili hii, ni muhimu kumjulisha mhudumu wa afya ili kuweza kujadili ni jinsi gani ataweza kutumia dawa hizo, kwa sababu dalili hii ni mbaya kiafya kwa mtu mwenye historia ya ugonjwa wa Kushuka Moyo (Depression).
Adhari nyingine ya dawa hizi ni kutokwa na uchafu ukeni. Baadhi ya wanawake, mara tu baada ya kutumia vidonge hivi hutokwa na uchafu ukeni, ikiwa ni pamoja na kupatwa na uwezekano wa kupungua au kuzidi kwa ute wakati wa tendo la ndoa. Ni muhimu sana mwanamke anapobaini dalili hizi, kuonana na mhudumu wa afya ili kubaini kama hali hiyo imesababishwa na athari ya vidonge au kuna maambukizi ya magonjwa ya zinaa.
Wanawake wengine huweza kujikuta wakikosa siku zao za hedhi baada ya kutumia vidonge vya uzazi wa mpango. Ingawa ugonjwa wa msongo wa mawazo (Stress), magonjwa, mchoko wa safari unaweza kusababisha hali hii, lakini inashauriwa kupima kama mtu amaepatwa na ujauzito hata kama anatumia vidonge hivi kama itatokea kukosa hedha katika mazingira tata.
Kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa ni athari nyingine inayoweza kumkuta mwanamke anayetumia vidonge vya uzazi wa mpango kutokana na vichocheo vilivyomo ndani ya dawa hizo, ingawa pia magonjwa kama ya kisukari, shinikizo kubwa la damu na kadhalika yanaweza pia kuchangia tatizo hilo.
Athari ya 10 na ya mwisho kwa wanawake wanaotumia vidonge hivyo, ni mabadiliko ya taswira ya kitu anachokiona mbele yake, hasa kwa wanawake wanaovaa miwani ya macho. Kwa kuwa macho ni moja ya eneo muhimu la ufahamu kwa mwanadamu, hali
hii inapowapata wanawake, inashauri kuonana mara moja na daktari wa macho pindi tu dalili hizi zinapoanza kujitokeza. Ni tahadhari gani mwanamke anatakiwa kuchukua kabla na baada ya kuanza matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango?
Kwa mwanamke mzazi, hairuhusiwi hata kidogo kuanza kutumia vidonge vya uzazi wa mpango ndani ya wiki tatu tu baada ya kujifungua mtoto au ikiwa atakuwa ananyonyesha mtoto mwenye umri wa chini ya miezi sita.
Aidha, ikiwa mwanamke amefanyiwa upasuaji mkubwa wa aina yoyote katika siku za karibuni, au kama mwanamke husika ni mvutaji wa sigara na ana umri wa zaidi ya miaka 35, haruhusiwi kutumia vidonge hivyo, kama ambavyo pia haruhusiwi kufanya hivyo mwanamke mwenye historia ya ugonjwa wa ini, manjano, moyo, saratani ya matiti, tumbo la uzazi pamoja na shinikizo la damu linalobadilikabadilika kila wakati kwa viwango vya 140/90 au zaidi, na au kama ana historia ya maumivu makali ya kichwa.

Madhara ya Heroin kwa wajawazito

Yafahamu madhara ya Mirungi

Cocain na madhara kwa mtumiaji na jinsi ya kumsaidia

BANGI INAVYOINGIZWA KATIKA MAGEREZA

Tuesday, July 14, 2015
MTAMBUE JUMA NKAMIA KUTOKA UANDISHI WA HABARI HADI NAIBU WAZIRI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete alimuapishe Juma Nkamia kuitumika Serikali kama Naibu Waziri katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Kwa taaluma, Naibu Waziri Nkamia (Pichani) ni mwanahabari ambaye amesomea na kufanya kazi ya habari kwa kipindi kirefu kabla ya kuingia katika Ubunge ambao umemuwezesha kuteuliwa kuwa waziri.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili katika wizara hiyo, Nkamia alisema anamshukuru Rais Kikwete kwa kumteua na kumpa dhamana hiyo na kuahidi kuwa atasaidiana na Waziri wa wizara hiyo kutimiza majuku ya wizara katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya nne.
“Kama kiongozi mwenye mamlaka ndani ya wizara hii, nipo tayari kushirikiana na viongozi wenzangu katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Idara zote zinazounda wizara hiyo”, alisema.
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inaundwa na idara kuu nne za kisekta ambazo ni Idara ya Habari, Idara ya Vijana, Idara ya Maendeleo ya Utamaduni na Idara ya Maendeleo ya Michezo.
Kwa kuwa tasnia ya habari ni miongoni mwa idara zilizo chini ya wizara hii, Nkamia alisema kuwa yupo tayari kushirikiana na wadau wa habari ikiwemo kusimamia maslahi ya waandishi wa habari nchini.
“Ukitaka kujua umuhimu wa vyombo vya habari na waandishi wa habari katika nchi yeyote ile, jaribu kuvifanya vyombo hivyo kuanzia redio, televisheni na magazeti visifanye kazi hata kwa muda wa saa moja tu uone ni hasara kiasi gani na hatari kiasi gani zitatokea katika nchi ile” alisema Nkamia.
Alisema anaheshimu na anatambua umuhimu wa vyombo vya habari na waandishi wa habari nchini na atafanya nao kazi vizuri kwa kipindi chote atakachokuwa wizarani hapo.
Alisema kuwa anatambua kuwa waandishi wa habari wanafanya kazi katika mazingira magumu wakati wa kutekeleza majukumu yao ikiwemo tatizo la “ukanjanja” na lugha mbalimbali zinozotolewa juu yao.
Amaeahidi kushirishirikiana na viongozi na wadau wa habari kuhakikisha kinaundwa chombo (bodi) kitakachosimamia maslahi ya waandishi wa habari.
Bodi itakayoundwa itasaidia kusimamia tasnia ya habari na kuhakikisha habari zinazoandikwa zitakuwa kwa maendeleo, manufaa na maslahi ya taifa na kuhakikisha inawajengea heshima waandishi wenyewe kwa kazi zao wanazofanya kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao na ya nchi.
Naibu Waziri Nkamia ametoa rai kwa wadau wote wa habari kushirikiana ili kufanikisha uundwaji wa sheria ya habari. Alisema “Sheria hii ikikamilika itasaidia kuboresha baadhi ya changamoto za wanahabari ikiwemo ajira zao na mafao yao ya sasa na uzeeni”.
Nkamia amepewa wadhifa huo baada ya Rais Dkt. Kikwete kufanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri katika kuziba nafasi zilizoachwa na mawaziri wanne waliojiuzulu na mmoja aliyefariki mwanzoni mwa mwezi huu.
Nkamia ni mkongwe aliyebobea katika taaluma ya uandishi wa habari akiwa amefanya kazi na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi.
Aliajiriwa kwa mara ya kwanza na Redio ya Taifa (Radio Tanzania Dar es Salaam) mnamo Oktoba 10, 1994 kama mwandishi msaidizi. Alifanya kazi RTD kwa muda wa miaka tisa hadi 2003 alipojiunga na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
Akiwa BBC Nkamia alifanya mambo mengi mazuri yaliyomjengea heshima mwenyewe na taifa. Ikizingatiwa kuwa Nkamia alipenda sana kutangaza habari za michezo, alifanikiwa kutangaza mechi mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Kama mwandishi wa habari za michezo, Nkamia alikuwa Mwafrika na Mtanzania wa kwanza kutangaza mchezo wa mpira wa miguu wa ligi ya Uingereza kwa lugha ya Kiswahili.
Kutokana na umahiri wake katika kutangaza habari za michezo, Nkamia aliaminiwa kutangaza mchezo wa fainali ya ligi ya Uingereza mwaka 2006 kati ya Manchester United na Arsenal na mwaka huo huo, BBC ilimpa tena jukumu la kutangaza mechi ya fainali ya Ligi ya klabu bingwa ya Ulaya kati ya Arsenal na Barcelona.
Mwaka 2006 Nkamia alirudi nyumbani Tanzania na kujiunga na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo alifanyakazi kama mwandishi na mhariri hadi 2009.
Mwaka 2009 hadi 2010 Nkamia alifanya kazi ya uandishi katika shirika la utangazaji la Sauti ya Amerika (VOA) inayomilikiwa na Taasisi ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kazi ambayo aliifanya kwa mwaka mmoja.
Mwaka 2010 Nkamia alitambua na kuitikia dhamiri yake ya kuitumikia nchi yake katika mambo ya siasa hivyo aliamua kurudi Tanzania kuomba ridhaa ya wana Kondoa Kusini awe mwakilishi wao bungeni na Kamati Kuu ya chama chake, Chama cha Mapinduzi, ikapitisha jina lake kuwa mgombea ubunge wa chama hicho jimboni humo.
Nkamia anasema, kwa kuwa alikuwa anafanya kazi na watu, wapo waliomshagaa kuacha kazi ya maslahi zaidi na kurudi nyumbani. Miongoni mwa hao ni Dkt. Shaka Ssali mtangazaji na mmoja wa wanahabari maarufu duniani aliyeuliza Nkamia anafanya nini katika karne yenye changamoto ya ajira duniani kuacha kazi yenye mshahara na maslahi makubwa na kwenda kwenye siasa.
Anasema kwake jibu la swali hilo lilikuwa rahisi kuwa ni Uzalendo wa nchi kwanza ndiyo maana aliamua kurudi kutoa mchango wake kwa maendeleo ya watu wake wa Kondoa Kusini na nchi kwa ujumla.
Kwa kuzingatia ukomavu na weledi alionao kwenye taaluma ya habari, ndiyo maana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete ameamini na kumpa dhamana ili asaidiane na Waziri mwenye dhamana katika Wizara hiyo, Fenella Mukangara, kuiongoza Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Nkamia amechukua nafasi hiyo badala ya Mhe. Amosi Makalla aliyehamishiwa Wizara ya Maji.
Wengine waliowahi kushika nafasi ya Naibu Waziri katika wizara hiyo ni Dkt. Makongoro Mahanga, N. Nswanzungwanko, Joel Bendera, Dkt. Emmanuel Nchimbi na Dkt.Fenella Mukangara ambaye sasa ni waziri wa wizara hiyo.
Juma Nkamia ni mtoto wa tatu kuzaliwa kati ya watoto sita wa familia ya Mzee Selemani Nkamia na Mwanaidi Ndwata. Anatokea eneo la kanda ya Kati katika mkoa wa Dodoma wilayani Kondoa. Ni baba wa familia mwenye mke mmoja Bi Amina na watoto wawili ambao ni Kassi mwenye umri wa miaka 13 anayesoma kidato cha pili Shule ya Sekondari ya Wavulana Fezza na Hassani mwenye umri wa miaka saba anayesoma darasa la pili katika shule hiyo hiyo.
CHAMA CHA MAPINDUZI NA HISTORIA YAKE.
Chama cha Mapnduzi CCM kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mfumo wa vyama vingi hauwi sababu ya chuki na msambaratiko wa umoja wa
kitaifa, amani na mshikamano. Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama tawala nchini Tanzania. CCM ilizaliwa 5 Februari 1977 baada ya kuungana kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa kikitawala Tanzania Bara na Afro-Shirazi Party (ASP) kilichokuwa chama tawala cha Zanzibar wakati huo. Chama cha Mapinduzi kilikuwa kikiongozwa na Mwalimu Nyerere na Afro-Shiraz Party kilikuwa chini ya Amaan Karume. Kwa miaka mingi CCM ilikuwa ikifuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Itikadi hii ilipewa nguvu za kisera mwaka 1967 lilipotangazwa Azimio la Arusha. Kutokana na azimio hilo uchumi uliwekwa mikononi mwa umma. Itikadi hii pia ilisisitiza umuhimu wa kuishi pamoja hasa katika vijiji vya Ujamaa.
MAUMIVU YA TUMBO KWA WANAWAKE (Natural home remedies for Endometriosis)
Endometriosis:
• Endometriosis is a common health disorder affecting women
• The condition can cause problems in conceiving
Symptoms to look for:
• Painful periods
• Painful cramps during menstruation
• Pain in the lower abdomen
• Pain during sexual intercourse
• Painful bowel movement
Causes:
• Certain cells, which are supposed to grow in the womb lining, start to grow outside the uterus, leading
to this condition
Natural home remedy using milk and asparagus powder:
1. Take 1 glass of warm milk
2. Add 2 tsp of Indian asparagus powder
3. Mix well
4. Drink 2 times a day
Natural home remedy using the Ashoka tree's bark:
1. Crush the bark of an Ashoka tree to powder, commonly available at ayurvedic stores
2. Take 2 tbsp of this powder
3. Mix it in 250 ml of water
4. Heat this water till only half the liquid remains
5. Strain the liquid
6. Drink 2 times a day
Natural home remedy using flax seeds:
1. Take 4 tbsp of flax seeds
2. Soak them in 1 cup of water overnight
3. Strain and drink this water the next morning
Tips:
• Drink pineapple juice to quicken the healing process
- See more at: http://mtsimbe.blogspot.com/2013/06/maumivu-ya-tumbo-ya-wanawake-natural.html#sthash.EMYO14go.dpuf
TIBA YA KUTOKA DAMU KWENYE FIZI
Pyorrhea:
• Pyorrhea is an advanced stage of gum disease
• It's a painless disease and hence goes undetected
Symptoms to look for:
• Dark red gums
• Bleeding in gums
• Bad breath
• Tooth loss
• Pus in gums
Causes:
• Neglecting dental hygiene gives rise to bacteria which leads to infection
• Incorrect eating habits
• Brushing aggressively
Natural home remedy using orange or lemon peels:
1. Take some orange or lemon peels
2. Rub on the gums for 5 min
3. Do this 2 times a day
Natural home remedy using pomegranate, salt and pepper:
1. Take 2 tsp of crushed pomegranate
2. Add ½ tsp black pepper
3. Add 1 tsp salt
4. Mix well
5. Apply this paste on the gums
6. Massage for 5 min
7. Gargle with lukewarm water
If pomegranate is not available, apply mixture of salt and pepper
Natural home remedy using spinach and carrot:
1. Take a handful of spinach leaves
2. Add 1 chopped carrot
3. Crush the two and make a paste
4. Press the paste on a sieve and extract its juice
5. Drink this juice 3 times a day
Tips:
• Eat 1 bowl of chopped cabbage and 1 banana every day. They both have nutrients which help improve
gum disease
Wednesday, July 1, 2015
YATAMBUE MAGONJWA YA NGONO UYAEPUKE
Mfumo wa uzazi unaweza kuathiria na mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na magonjwa ya ngono ambayo hushambulia mfumo huo, leo tutajadili baadhi ya magonjwa hayo ambapo tutapata kujua majina yao, jinsi yanavyoambukizwa, dalili na kinga au tiba zao ijapokuwa kipengele cha tiba sitakiongelea kwa undani.
1. KISONONO:
Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya kujamiiana na mtu mwenye maambukizi na hushambulia zaidi sehemu za siri za jinsia zote.
Dalili;
Dalili kuu za ugonjwa huu ni mgonjwa kutokwa na usaa kwenye sehemu za siri na mgonjwa kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja ndogo, na ukikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa huenea zaidi kwenye viungo vingine vya uzazi.
Kuzuia/Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni kuacha kujamiiana au kutumia kondom kwa kila tendo la ngono.
na kwa wale ambao tayari wanamaambukizi wanashauriwa kutibiwa wote hospitalini na kuacha kufanya ngono hadi wapone.
2. KASWENDE:
Huu ni ugonjwa wa ngono unaosababishwa na bakteria.
Dalili;
Mgonjwa wa Kaswende hupata mwasho mkali sehemu za siri na kupata vijeraha vidogo vidogo sehemu hizo na akikaa sana na ugonjwa huo bila kutibiwa huweza kuathirika sehemu zingine za mwili kama vile, Moyo, ubongo na hatimaye kusababisha kifo.
Kinga/ Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni; kuacha kujamiiana na ukishindwa kuacha kabisa basi fanya ngono iliyo salama(yaani utumie Condom)
Ugonjwa huu hutibiwa Hospitalini na inashauriwa wenza wenye ugonjwa huu watibiwe kwa pamoja.
Wakati wa matibabu maswala ya kujamiiana yawekwe kando hadi matibabu yakamilike kwani yanaweza yakaongeza maambukizi mapya.
3. KLAMEDIA:
Huu ni mojawapo ya magonjwa ya ngono ambao haujafahamika unaambukizwa na wadudu wa aina gani.
Dalili;
Mgonjwa wa klamedia hutokwa na uchafu katika sehemu zake za siri na kupata maumivu makali wakati wa haja ndogo na wakati wa kujamiiana.
Kinga/Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni sawa na kinga ya magonjwa mengine ya zinaa, ili usiupate ugonjwa huu unashauriwa kuacha kabisa kufanya ngono au kutumia condom kwa kila tendo la ndoa.
Hugonjwa huu pia hutibiwa hospitalini.
4. TRIKOMONA:
Ugonjwa huu husababishwa na protozoa (trikomonasi vaginalis) ambazo huambukizwa kwa njia ya kujamiiana.
Dalili;
Dalili za ugonjwa huu hutofautiana kwa kila jinsia.
WANAWAKE: Wanawake wenye ugonjwa huu hupatwa mwasho mkali katika sehemu za siri,
Hutokwa na uchafu wa rangi ya njano au kijani wenye harufu mbaya sehemu za siri.
WANAUME: Wanaume wenye ugonjwa huu hupata maumivu makali wakati wa haja ndogo.
Kinga/ Tiba;
Ugonjwa huu pia unazuilika kwa kuacha kujamiiana au kutumia condom kwa kila tendo la ngono.
Mgonjwa atatibiwa hospitalini na kupona kabisa.
CHAKULA WAKATI WA MIMBA
Madaktari wengi wanashauri kunywa madawa ya vitamin sababu wajawazito wengi hawali vizuri. Madini ya muhimu kwa mtoto ni kama yafuatayo; Calcium, Iron, Folate (B vitamin). Haya madini yote yanaweza kupatikana kwenye vyakula vifuatazo;
Calcium:
Mtoto anahitaji Calcium kwa ajili ya kukuza viungo vya mwili na mifupa kukomaa vizuri. Mwili wako unanyonya Calcium inayohitajika na mtoto hivyo basi unahitaji kula vyakula vitakavyoongeza kiasi hichi mwilini. Lakini pia ili Calcium inyonywe na mwili unahitaji kukaa juani kwa kipindi kama cha dakika kumi kila siku. Calcium hupatikana kwenye, maziwa, mboga za majani kwa wingi, Mayai (Hakikisha yameiva vizuri )Samaki (esp mifupa lakini sio samaki wote wanashauliwa kula wakati wa mimba), maharage ya soya, na mchele.
Madini ya Chuma (Iron)
Chuma ni muhimu kwa utengenezaji wa damu, kwani kipindi hichi damu nyingi inahitajika kwa ajili ya kumpelekea mtoto chakula. Wajawazito wengi huwa vichanga vyao vinakufa sababu ya ukosefu wa damu toka kwa mama. Iron hupatikana toka kwa vyakula kama; Mboga za majani kwa wingi zaidi (Matembele yana Iron zaidi, mchicha, brocolli, sukuma wiki n.k). Chai na Kahawa huwa inasaidia kuzuia kunyonywa ka iron mwilini hivyo epuka kunya chai nyingi na ikiwezekana uache kunywa kahawa kwa kipindi hiki.
UGONJWA WA KIFAFA KWA WATOTO (seizures)
Kifafa mara nyingi husababishwa na uvujaji wa wave za kama za umeme (electrical discharge) kwenye ubongo ama husababishwa na hali ya kuzimia (baada ya kupunguka kwa msukumo wa damu ubongoni). Dalili (symptoms) zinaweza hutofautiana kulingana na sehemu ipi ya ubongo imehusika, lakini mara nyingi utasikia hali ya mwili kusisimka sio kwa kawaida, misuli kuvutika/kukaza yenyewe, na pia kupoteza fahamu.
Baadhi ya vifafa vingine huwa ni matokeo ya magojwa mengine mwilini, kama upungufu wa sukari kwenye damu, maambukizi, kuuumia kichwa(head injuries), ajari za barabarani au kuoverdose madawa ya kulevya. Pia kifafa kinaweza sababishwa na uvimbe kwenye ubongo ama tatizo linguine la afya linaloathiri ubongo. Kifafa mara nyingi hutokea zaidi ya mara moja.
Watoto wa chini ya miaka 5 huwa wanapata hali ya kifafa pale joto lao la mwili linapozidi degree 38 (100.4° F (38° C) aina hii ya kifafa inaitwa Febrile seizure. Hii inaogopesha kama mzazi lakini hii hali ni ya dakika chache tuu, mara chache husababisha matatizo makubwa, especially kama joto hili limesababishwa na maambukizi kama meningitis.
Kwa watoto chini ya miaka 5, kuhold pumzi inaweza sababisha hali ya kifafa (seizure). Kuna watoto wakati wanapokasirika huwa wanashikiria pumzi (hawavuti pumzi kwa sekunde chache) kabla tuu ya kuachia kilio kikubwa, kabla ya kupoteza fahamu kifafa kufuatia. Mara nyingi hali hii huisha yenyewe.
Watoto wa umri zaidi ya miaka 5 wachache huwa na hali hii lakini mara nyingi huwa inaisha baada ya sekunde chache.
Kama mtoto wako ana kifafa ufanyeje
Kama mtoto wako amepatwa na kifafa basi unashauriwa kumlaza chini sehemu ambayo ni salama, wanashauri umlaze upande wake wa kulia. Ondoa kitu chochote cha hatari ambacho kipo karibu, kama vyupa, sindano, mawe n.k. Kama ana cheni shongoni ivue ama kama nguo ipo shingoni ivue pia isimkabe. Usijaribu kupanua mdomo wa mtoto anapokuwa na kifafa ama kuweka kitu mdomoni kwake, pia usijaribu kuzuia kuweweseka kwake.
Mara tuu kifafa kinapoisha basi mfariji mtoto, ni muhimu kwa watoto kubaki kulala chini mpaka hali hii iishe kabisa nay eye mwenyewe akitaka kuinuka.
Tafadhari mwite daktari pale ambapo kifafa kinaendelea zaidi ya dakika 5, pia kama mtoto ana vitu vifuatavyo:
. anashindwa kupumua
.ameumia kichwa
.ana magonjwa ya moyo
.hajawahi kupata kifafa zamani
.kama amekunywa sumu ama ameoverdose dawa.
Baada ya kifafa, mtoto huonekana kuchoka, amechanganyikiwa, na anaweza kulala usingizi mzito sana (postictal period) hauhitaji kumwamsha mtoto as long as anapumua vizuri. Usijaribu kump chakula mpaka mtoto aamke na aonekane kuchangamka.
TATIZO LA KUTOKULALA KWA WATOTO WACHANGA
Watoto wengi wadogo huwa wanapata shida sana kutulia na kulala wakati wa usiku. Kwa watu wengine hili sio tatizo kwao na kama haikusumbui mtoto wako kwenda kulala muda ambao wewe unaenda kulala, basi sio shida. Lakini, kama wewe, ama mtoto wako anasumbuka na tatizo la kushindwa kulala usiku unaweza kujaribu kufanya yafuatayo:
Kila mtoto ni tofauti na fanya tuu kile unachoona kinafaa kwa mwanao.
Kama Mtoto wako hataki kwenda kitandani:
Amua saa ngapi ama mda gani unataka mtoto awe anaenda kitandani.
Kwa kuanza, mda wa mtoto kwenda kulala ukikaribia (ule mda anaolalaga kila siku) anza kumpeleka kulala dakika 20 kabla kwa siku ya kwanza, alafu siku ya pili mpeleke dakika 30 kabla, ya tatu iwe dakika 40 kabla na kuendelea kuongeza dakika 10 kila siku mpaka ifikie mda ule unaotaka wewe.
Jipangie kikomo cha kukaaa na mwanao kitandani wakati wa kulala, mfano msomee hadithi moja tuu, alafu sema usiku mwema, muage na kumwacha alale.
Mpatie mtoto wako toy yake anayoipenda alale nayo, mfano kama huwa anatumia dummy ya mdomoni, ama kitaulo (kuna watoto hunyonya kitaulo) ama chochote kitakachombembeleza kulala.
Kama mtoto wako analia, umwache kitandani na uondoke chumbani na mpatie dakika 5 mpaka 10 ya kujituliza mwenyewe kabla ya kumyamazisha tena.
Usimnyanyue ama kumbeba mtoto, ama kumtoa kitandani na kama mtoto atainuka na kutoka kitandani basi mchukue na kumrudisha kitandani tena.
Washa taa yenye mwanga mdogo (kama unayo) ama acha mwanga wa mbalamwezi uingie kama kutakuwa na ulazima huo.
Hakikisha amelala kabla ya kwenda kumwangalia mtoto ili usimwamshe tena.
Fanya hivi kila siku na usikate tamaa baada ya siku moja tuu, jipatie siku 5 ili mtoto awe na mazoea.
Kama mtoto anaamka mara kwa mara usiku.
Ni kawaida kwa watoto wa zaidi ya miezi 6 kulala usiku mzima bila kuamka, Hata hivy, kuna watoto wengi chini ya miaka mitano huwa hawalali usiku mzima bila kuamka. Kuna ambao watarudi kulala tena wao wenyewe na wengine ambao watalia kwa kutaka uwepo wa mtu.
Kama hii hali itatokea, jaribu kutatua tatizo linalimfanya mwanao aamke usiku.
Je ni njaa? kama mwanao ni mkubwa zaidi ya mwaka moja, maziwa na uji huwa yanaweza mfanya alale usiku mzima kama hivyo ndio alikunywa mda tuu kabla ya kulala.
Je ni uoga/hofu ya giza? unaweza kutumia taa za usiku ama unaweza acha taa ya corrido iwake usiku.
Je ni ndoto mbaya? kama ni hivyo jaribu kutafuta kama kuna kitu kinachowasumbua ambacho ndio husababisha kuota usiku.
Je ni joto/ baridi kali? kama ni hivyo punguza ama uongeze nguo za kujifunika ama punguza/ongeza joto ama baridi kwenye chumba kwa kufungua milango ama kupunguza AC.
Kama hakuna sababu maalumu inayomfanya mwanao aamke, alie ama kutaka ukae nae usiku basi jaribu yafuatayo:
Mda wa kuamka - kama mwanao huamka wakati huo huo kila usiku basi jaribu kumwamsha kati ya dakika 15 mpaka 60 kabla alafu mbembeleze tena kurudi kulala.
Mruhusu mtoto alale chumba kimoja na kaka yake ama dada yake kama tatizo ni kuogopa kuwa peke yake. Hii itawasaidia wote walale usiku mzima.
Mfundishe mwanao kujirudisha kulala yeye mwenyewe usiku, kwanza kama kila kitu kiko sawa, mmbembeleze mwanao kulala bila ya kuongea nae sana akiwa kitandani. Kama anataka kinywaji mpe maji ila angalisho usimpatie chakula wakati akiwa ameshtushwa na usingizi. Ili njia hii ifanye kazi ni lazima umwache mtoto kitandani na usimnyanyue na kwenda nae sebuleni, ama chumbani kwako. Mwache alie kwa kati ya dakika 5 hadi 10 ndipo ukamwangalie tena. Mwambie arudi kulala na mwakikishie kwamba hakuna kitu cha kuogopesha na usiongee nae kitu kingine, kama ni mtoto mchanga mbembeleze kwa kumpapasa mgongoni akiendelea kulia mbebe kwa dakika 2 tuu alafu mrudishe kitandani. mwache kama analia ikifika dakika 10 nenda tena, fanya kama hapo juu na umwache ena ajirudishe kulala. Endelea hivyo kwa siku kadhaa na mtoto atazoea na kuanza kusinzia mwenyewe ukimweka kitandani.
Msaidiane na mumeo, mnaweza mkafanya zamu ya kumwangalia mtoto anapolia, hii pia husaidi mtoto kuwajua na kuwazoea wazazi wote wawili, pia itamfanya mama asichoke sana.
Ndoto za kutisha
Ndoto za kutisha ni kawaida kabisa. Wao mara nyingi huanza kati ya umri wa miezi 18 na miaka mitatu. Ndoto hizi ni si kawaida ni ishara ya masumbuko ya hisia. Huwa inaweza kutokea kama mtoto wako ana wasiwasi juu ya kitu au amepata hofu na kipindi ama hadithi aliyoangalia kwenye luninga. Baada ya ndoto, mtoto wako atahitaji faraja na uhakika. Kama mtoto wako anaota ndoto hizi sana na hujui ni kwa nini basi ongea na daktari.
Kuweweseka usiku
Hutokea kabla ya umri wa mwaka moja ingawa pia ni kawaida zaidi kwa watoto kati ya umri wa miaka mitatu hadi nane. mara nyingi mtoto huweweseka na kupiga kelele ama kupigapiga mikono na miguu akiwa bado yupo usingizini. hutokea baada masaa machache ya kulala, wanaweza kukaa na kuongeaongea wakiwa usingizini na kuonekana wenye hofu wakiwa usingizini. Wala usiogope na mtoto wako itafika wakati itapita tuu.
Usimwamshe mwanao wakati akiweweseka ila kama hutokea mda huohuo kila usiku basi jaribu kumwamsha dakika 15 kabla ya muda ule anaoweweseka kila siku. abaki macho kwa dakika chache kabla ya kumrudisha kulala tena.
FUNGUS WAKATI WA MIMBA (thrush)
Ni kawaida kabisa kutokwa na majimaji mazito (vaginal discharge) ukeni wakati ukiwa na ujazito. Usiwe na wasiwasi kama majimaji haya ni myepesi na yana muonekano wa rangi ya maziwa.
Dalili za kuwa na fungus ukeni:
· Majimaji yakiwa mazito, myeupe na rangi ya maziwa, na yanayoonekana kama cottage cheese, ama maziwa ya mgando, ama yaliyoharibika.
· Kama unawashwa, na kusikia kuvimba kama vile umejikwaruza, na muonekano wa uwekundu sehemu ya ukeni.
· Inauma wakati wa kujamiiana
· Unasikia kuchomwachomwa wakati unakojoa
Je nilipataje thrush:
Maambukizi ya ukeni wakati wa mimba ni ya kawaida. Thrush husababishwa na fungus (yeast) wanaoitwa candida albicans ambao wapo na huishi kwenye miili yetu bila kusababisha tatizo lolote. Wapo pia kwenye mfumo wa chakula na mara nyingi hawana madhara yoyote kwetu na wala hautojua kama wapo.
Huwa wanaleta tatizo pale tuu wakati fungus hawa na vijidudu vingine ndani na nje ya mwili vinapopungua ama kuongezeka kuliko kiasi kinachitakiwa. Unaweza kupata thrush pale ambapo:
· Unapokuwa mjamzito mabadiliko ya hormones kwenye mwili husababisha mwili uwe na sukari nyingi kuliko kiasi inayoitwa glycogen ambayo husababisha fungus kuzaliana kwa wingi (wanatumia glycogen kama chakula na hivyo kuwapatia nguvu ya kujiongeza idadi).
· Unapotumia antibiotics, dawa hizi huua vijidudu mwilini ambapo pia huua vijidudu vizuri vinavyopigana na vile vibaya, hivyo basi balance ya vijidudu hivi inakuwa imebadilika na hiyo kusabaisha vile vibaya vizaliane kwa nguvu.
· Kisukari (Diabetes): kama una ugonjwa wa kisukari ambacho huujakicontrol pia husababisha thrush.
· Kama immune system yako ni dhoofu. Hii inaweza kutokana na pia na matibabu ya magonjwa kama sarakani (cancer) ama magojwa na HIV.
Ingawa thrush sio magonjwa ya zinaa, yanawezekana kuambukizwa kama partner wako amepata maambukizi haya, hivyo mnashauriwa wote wawili mpate matibabu kwa wakati moja.
Kama unafikiria una thrush, tafadhari mwone daktari.
Daktari atakupatia dawa, ingawa wanashauri kutotumia chochote kipindi cha mlongo wa kwanza wa mimba (miezi 3 ya mwanzo) .
Dawa zingine ni za kuweka ukeni (kidonge), unashauriwa kuweka usiku wakati umelala ili inyonywe vizuri wakati umelala. Thrush ni vigumu kupona upesi hivyo basi ni vyema umalize dozi utakayopewa na daktari. Tafadhari usichukue dawa za vidonge ambayo utahitaji kumeza, bado haijajulikana kama vina madhara gani kwa mtoto.
Je nifanyeje
· Wakati unapojiosha ukeni, usitumie sabuni osha na maji masafi (sio ya kisima) ikiwezekana jichemshia maji kidogo tuu(kuua vijidudu) kwa ajili ukeni. Na ikiwezekana jioshe mara moja kwa siku kwani kujisafisha sana ukeni unaondoa wale wadudu wanaohitajika kulinda uke (Good Flora microorganism).
· Usitumie mafuta yatakayoirritate ngozi kama pedi za kunukia, deodorant za ukeni, na sabuni zakunukia.
· Kula maziwa mgando yasiyo na sukari, ama ingiza maziwa ya mgando ukeni.
· Kama utatumia maziwa mgando, njia rahisi ya kuweka ukeni ni kwa kutumia tampoo, chovya tampoo kwenye maziwa mgando, dumbukiza tampoo ukeni, iache kwa muda wa lisaa limoja, alafu itoe.
· Kupunguza kueneza thrush, basi jifute toka mbele kwenda nyuma kila baada ya kutumia choo.
· Vaa chupi za cotton 100%
· Wakati wa kujamiiana tumia kilainisho(lubricant) kupunguza maumivu kama una thrush.
Je thrush itamfikia mtoto tumboni
Hapana, mtoto amefunikwa na mfuko na hatadhurika.
Hata hivyo ni muhimu kupata matibabu kabla ya kujifungua, kwani mtoto anaweza kuambukizwa wakati akitokea ukeni.
Kama hii ikitokea basi utahitaji matibabu wewe na mtoto, mtoto mara nyingi anakuwa na utando mweupe kwenye ulimi.
Utagundua thrush huja na kuondoka wakati wa mimba, na huchukua mda mrefu kuitibu lakini sio kitu cha kuogopa sana.
KUTAPIKA NA KUHARISHA KWA MTOTO
Ni kawaida kwa watoto wachanga na watoto kutapika. Katika kesi nyingi , kutapika hudumu kati ya siku moja mpaka mbili na si ishara ya kitu chochote kikubwa . Kawaida sababu ya kutapika kwa watoto ni gastroenteritis . Haya ni maambukizi ya kolomeo kawaida husababishwa na virusi au bakteria. Na pia husababisha kuhara . Mfumo wa kinga ya mtoto wako kwa kawaida hupigana na maambukizi baada ya siku chache.
Watoto mara nyingi pia hutapika wakati wanapomeza hewa wakati wa kulishwa . Hata hivyo , kuendelea kutapika wakati mwingine inaweza kuwa ni ishara ya kitu kibaya zaidi , ikiwa ni pamoja maambukizi makali kama vile uti wa mgongo.
Ukurasa huu unaeleza nini cha kufanya kama mtoto wako anaendelea kutapika na iuaelezea baadhi ya sababu ya kawaida ya kutapika kwa watoto wachanga, na watoto kwa ujumla . Kama mtoto wako ana joto la juu , unaweza pia kusoma kuhusu homa kwa watoto
Nini cha kufanya.
Kama mtoto wako anatapika, unapaswa kufuatilia hali kwa uangalifu mkubwa. Amini moyo wako na mpeleke kwa dakitari wako mara moja kama wewe una wasiwasi.
Kama sababu ni tummy bug tuu (kuhara kwa kawaida kwa mtoto ama tummy flu), atakula na kucheza kama kawaida. Katika kesi hiyo, endelea kumlisha kama kawaida na kumpatia kinywaji (maji, juice n.k) mara kwa mara. Maji humsaidia kutopunguka kwa uwingi wa maji mwilini ambao ni hatari.
Lakini kama haonekani wa kawaida, - kwa mfano, kama yupo floppy , hasira , kutojibu, au amepoteza hamu ya kula - inawezekana anaumwa, hivyo unapaswa kuwasiliana na daktari wako mara moja.
Kumpeleka kwa daktari
Unapaswa kuwasiliana na daktari wako kama :
•Mtoto wako amekuwa akitapika kwa zaidi ya masaa 24
• Mtoto wako anatapika ndani ya masaa nane, au kama unafikiri amepungukiwa na
maji mwilini.
• Kama ni floppy, mwnye hasira, anagoma chakula , au hayupo kwenye hali ya kawaida
, • Ana maumivu makali tummy
• Ana maumivu ya kichwa na shingo ngumu.
Ishara ya upungufu wa maji mwilini
Kutapika kali na kuhara kunaweza kwa urahisi kusababisha upungufu wa maji mwilini , hasa katika
watoto wachanga. Hii ina maana mwili wa mtoto wako hana maji ya kutosha mwilini au hana chumvi inayohitajika kwa ajili ya mwili kufanya kazi kwa kawaida .
Watoto wenye upungufu wa maji mara nyingi hujisikia na huonekana kuumwa.
Ishara ya upungufu wa maji mwilini ni :
• kinywa kikavu
• kilio bila kutoa machozi
• kukojoa kidogo sana au kiasi cha nappies anazokojolea kupunguka.
• Kuongezeka kwa kiu
• Kudhoofika
Ufanyaje
Jambo muhimu zaidi unaweza kufanya kama mtoto wako anatapika ni kuhakikisha anaendelea kunywa maji ya kunywa.
Kama mtoto wako anatapika , endelea kumnyonyesha. Kama wamepungukiwa maji, , atakuwa anahitaji maji ya ziada. Uliza mfamasia wako kama wangeweza kupendekeza kumpatia dawa ya kusaidia kutopunguka kwa maji mwilini.
Dawa hii ni poda maalum unaitengeneza kwa kuweka kwenye maji. Ina sukari na chumvi katika kiasi maalum ya kusaidia kuchukua nafasi ya maji na chumvi kupotea kwa njia ya kutapika na kuhara.
Watoto ambao hutapika wanapaswa kunywa maji haya kidogokidogo hivyo hawatapungukiwa maji
mwilini. .Pia motto anaweza kunywa maji , maji mengi kwenye juice ya kuchanganya na maji , diluted maji ya matunda au maziwa.
Hata hivyo, kama pia wanaharisha, maji ya matunda ziepukwe. Tena, GP wako au mfamasia anaweza kupendekeza ORS.
Dawa ya kusaidia wakati wa kuharisha kwa motto.
Sababu ya kutapika kwa watoto.
Kuna sababu ya uwezekano wa kutapika katika watoto, ambayo ni ilivyoelezwa hapo chini
gastroenteritis
Gastroenteritis ni maambukizi ya utumbo. Ni kitu cha kawaida inayosababisha kutapika kwa watoto na kwa kawaida huchukua muda wa siku chache .
maambukizo ya hatari
Watoto wadogo hasawapo katika hatari ya kupatwa na maambukizi kama vile pneumonia au maambukizi ya figo. Unapaswa kuwasiliana na daktari wako kama motto ana dalili ya magonjwa haya.
ugonjwa wa kidole tumbo
Ugonjwa wa kidole tumbo
Friday, June 26, 2015
RAHA!!!!!! JUA VYAKULA VINAVYOREFUSHA UUME>
If you want to increase the size of your penis, you are undoubtedly
doing penis enlargement exercises. However, to get the most benefit from
your workouts, you need to make sure that your body is well-nourished.
Eating the right foods will help with increasing penis size, improving
your sexual performance, and even improving the health of your penis and
prostate. Seven foods in particular will help you get faster and better
results from your penis enlargement program. Here we go
ALSO READ:8 FOODS THAT INCREASE 5EXUAL STAMINA
1) Cayenne Pepper
If you consume cayenne pepper (the seasoning or the pepper itself) each
day, you can strengthen your blood vessels and boost your metabolism.
ALSO READ:8 FOODS THAT INCREASE 5EXUAL STAMINA
2) Dark Chocolate
A small amount of dark chocolate daily can do a lot for your body,
including helping your penis grow bigger. Dark chocolate helps you
increase your size since it contains flavonoids, which improve
circulation.
ZITAMBUE SIRI NA FAIDA ZA KITUNGUU SWAUMU
Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum. Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba.
Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen'genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu.
Historia inaonesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika China mwaka 510 K.K na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Roma. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana.
Mwaka 1858, mtafiti na mwanasayansi wa nyakati hizo, Louis Pasteur aligundua uwezo wa kitunguu swaumu katika kuua vimelea mbalimbali vinavyosababisha magonjwa, na hivyo vikaanza kutumika kama dawa ya kusafishia vidonda na kuzuia kidonda ndugu hasa zama za vita ya kwanza na pili ya dunia. Isitoshe, mpaka sasa zipo dawa kadhaa zilizotengenewa kwa kutumia jamii hii ya vitunguu swaumu ikiwemo dawa ya kusafisha mdomo (mouth wash) ingawa watumaiji wake wengi huilalamikia dawa hiyo kwa sababu ya harufu mbaya ya dawa hiyo inayowasababishia kunuka kwa mdomo.
Faida za vitunguu swaumu
Katika tafiti mbalimbali vitunguu swaumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kutibu maambukizi ya bakteria, fangasi na virusi vya aina mbalimbali. Aidha husaidia kuzuia magonjwa ya moyo ikiwemo kuondoa lijamu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kurekebisha shinikizo la damu. Faida nyingine za vitunguu swaumu ni pamoja na
- Kutibu saratani ikiwemo saratani ya tumbo na utumbo mkubwa. Tafiti zinaonesha idadi ndogo ya wagonjwa wa saratani katika nchi ambazo wakazi wake wana utamaduni wa kutumia vitunguu swaumu kwa wingi.
- Vitunguu swaumu husaidia kudhibiti kiwango cha sukari katika damu. Hata hivyo inashauriwa kwamba wagonjwa wa kisukari wanaotumia sindano za insulin wasitumie kitunguu swaumu kwa wingi mpaka watakaposhauriwa na daktari.
- Huzuia kusanyiko la chembe sahani zinazosaidia kuganda kwa damu (platelet aggregation)
- Husaidia ufyozwaji wa thiamin, hivyo kusaidia kuepusha mwili na ugonjwa wa beriberi
- Ina kiasi kikubwa cha vitamini C ambayo husaidia kuzuia ugonjwa wa kiseyeye
- Hutumika kutibu magonjwa nyemelezi kama toxoplasmosis, hasa kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini.
Katika utafiti uliofanyika nchini Czech ilionekana kuwa matumizi ya vitunguu swaumu yalisaidia sana katika kupunguza kusanyiko la lijamu (cholesterol) pamoja na mafuta yasiyofaa mwilini (low density lipoproteins) katika mishipa ya damu. Aidha, mwaka 2007 BBC iliripoti matumizi ya vitunguu swaumu katika kusaidia kumkinga mtumiaji dhidi ya aina fulani ya mafua iliyosababishwa na virusi. Mwaka 2010, ulifanyika utafiti mwingine ambao ulijumuisha wagonjwa 50 wenye shinikizo la damu sugu ambalo lilikuwa ni vigumu kudhibitiwa hata kwa matibabu yaliyozoeleka ya dawa na njia nyingine. Kama njia ya kuchunguza ufanisi wa vitunguu swaumu katika kutibu shinikizo la damu, baadhi ya wagonjwa hao walipewa vitunguu swaumu wakati wengine walipewa dawa isiyohusika na matibabu ya shinikizo la damu (au placebo). Ilionekana kuwa wale waliopewa vitunguu swaumu kama dawa ya shinikizo la damu walionesha maendeleo mazuri kwa vitunguu swaumu kuweza kushusha vizuri kiwango cha shinikizo la damu, hususani systolic pressure, tofauti na wale waliopewa placebo.
Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida zilizoainishwa hapo juu ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa (ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na mambo yafuatayo;
- Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
- Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na kupunguza madhara ya kisukari.
- Iwapo vitapondwa pondwa vizuri, vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo Allicin ambayo ni dawa dhidi ya bateria, na phytoncide ambayo huua fangasi wa aina mbalimbali.
- Harufu mbaya ya kitunguuu swaumu hutokana na gesi aina ya hydrogen sulfide ambayo inayotolewa baada ya kuvila.
Ukiacha faida zake, vitunguu swaumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;
- Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
- Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
- Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
- Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
- Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.
- Aidha, vinaelezwa pia kuwa na madhara kwa wanyama jamii ya paka na mbwa.
Subscribe to:
Posts (Atom)